1 Thessalonians 4:13-16

13 aLakini ndugu, hatutaki mkose kujua kuhusu wale waliolala mauti, ili msihuzunike kama watu wengine wasiokuwa na tumaini. 14 bKwa kuwa tunaamini kwamba Isa alikufa na kufufuka, na kwa hivyo, Mungu kwa njia ya Isa atawafufua pamoja naye wale waliolala mautini ndani yake. 15 cKulingana na neno la Bwana mwenyewe, tunawaambia kwamba sisi ambao bado tuko hai, tuliobaki hadi kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia waliolala mauti. 16 dKwa maana Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni, akitoa amri kwa sauti kuu, pamoja na sauti ya malaika mkuu, na sauti ya tarumbeta ya Mungu. Nao waliokufa wakiwa katika Al-Masihi watafufuka kwanza.
Copyright information for SwhKC